Saturday, December 4, 2010

TUPELEKE CHOMBO ANGANi KiFiKRA

   
         Tanzania ni moja kati ya nchi ambazo zimebarikiwa utajiri mkubwa sana wa malighafi mbalimbali duniani, katika Afrika ni nchi ambayo ina eneo kubwa kuliko yote na lenye utajiri wa kila aina. Lakini ukiitazama Tanzania kati ramani ya dunia katika maendeleo Tanzania ni moja kati ya nchi zisizo tambulika ingawa zina malighafi za kutosha. Ukiutaja Mlima Kilimanjaro, Mbuga za wanyama za Ngorongoro na Serengeti pamoja na Ziwa Victoria utakuta kwamba ni majina yanayotambulika sana duniani.
      Waandishi wengi wa mashairi, wa  vitabu na wasanii wa filamu wamepata kujiongezea vipato katika nchi zao kwa kutumia majina ya nchi kama Tanzania, katika baadhi ya vitabu nilivyosoma mfano “Life on the Edge” mwandishi anaelezea hadithi yake alivyokuja kutembelea mbuga za wanyama za Serengeti, na katika filamu mfano ya Jimmy Carey anaelezea nyoka mbalimbali wanaopatikana Tanzania, na katika wimbo wa Nas na Damian Marley wanajivunia lugha ya Kiswahili kwa maneno “habari gani nzuri sana” hii inadhihirisha kua Tanzania inatambulika vizuri katika uso wa dunia kwamba kuna nchi iliyobarikiwa Afrika inaitwa Tanzania.
          Ingawa tumetambulika sasa isiwe tija lengo ni kwamba sisi vijana tuna malengo gani na nchi yetu ya Tanzania, kama vijana ni taifa la kesho! Je vijana wa leo tunalifikiria taifa la kesho? lengo sio kuwasomesha vijana kwamba tujivunie jina la Tanzania bali tujifikirie kama sisi vijana ni taifa la kesho, tufanyenini leo ili kesho tuweze kujivunia kua tulikua vijana wa taifa la leo. Huu ndo wakati wakulisongesha gurudumu la maendeleo katika taifa letu la Tanzania.
      Vijana wengi wa kitanzania hawajui haki zao hii imeonekana ni swala la kawaida, japokua vijana wengi wakitanzania wana akili pamoja na nguvu ila tatizo tumeshakua na mfumo tegemezi wa kimawazo katika  kujiendeleza.
       Kama kijana wa kitanzania akiwa huru kifikra leo Tanzania ya kesho inaweza kupeleka chombo mwezini, nasema hivyo kutokana na nguvu ya kufikiri tuliyonayo katika ubongo ni kubwa mno, tunaweza kuibadilisha dunia vile sisi tunataka kama tukitumia fikra  sahihi, na  kama vijana wa Tanzania tunataka kupeleka chombo angani basi tunaweza kukipeleka ila tunatakiwa tuwe huru kifikra ili tuwe na fikra sahihi katika kutimiza malengo ya taifa la kesho, kama unataka kwenda mahali usipopajua kifkra panakua mbali, ila kama unataka kwenda mahali unapopajua kifkra panakua karibu, sasa vijana mko wapi?
     Tuamkeni tujipange tunataka kwenda wapi, tusiwe wavivu wa kufikiri, Tanzania inabaki kichwa cha mwendawazimu, na sisi tunafurahia kuitwa wendawazimu? usijisemee kua wewe sio mwendawazimu labda kama haukubali misemo ya wahenga kwamba “akioza samaki mmoja, wote wameoza”. Ni wakati wakumtoa samaki aliyeoza na kuwatengeneza wale walio wazima ili waweze kutumika.
          Vijana nalia  na nyie, sisi  ndio tunaweza kuibadilisha Tanzania ya leo ili kesho ikaitwa Tanzania ya Wazalendo wa "next level" kama tunavyoupenda huo usemi. Sisi ndio tunaoweza kuipeleka Tanzania angani kifikra na kimatendo, najua wengi watashindwa kuielewa kauli hii ila ni wewe mwenye uwezo wa kufikiria mbali na ukafika mbali, ni wewe inayeweza kupeleka chombo angani kwa fikra za kimaendeleo ya kwako na taifa lako. Vijana wa Tanzania tunaweza tukiamua, tusipelekwe tu na mfumo nyonyevu wa fikra. Tubadilike sasa. Kumkichwa ni wewe!

Tuesday, November 9, 2010

hati miliki

Tuko kimya  kwani tunafuatilia maswala ya hati miliki kwa kua kuna mambo makubwa yatafanyika kupitia blog hii. Tuzidi kushirikiana kwa pamoja. Ahsanteni sana wana KUMKiCHWA

Friday, October 22, 2010

ZAiDi YA JiNA! ViPi HESHiMA?



Tunapotega masiko yetu katika redio lengo ni kujua nini kimejiri katika taifa letu kwenye taarifa ya habari, ama tunapotazama runinga zetu wakati wa taarifa ya habari lengo ni kujua nini kimejiri, wakati huu ndipo binadamu anapoheshimu hisia zake ili aweze kupata ujumbe au taarifa kwa wataalamu wa habari, na wengi wao hupata taarifa walizozitegemea kutoka katika chombo alichokiheshimu.
Sasa chombo hiki kimeheshimika kwasababu kinatoa taaarifa ya habari iliyo sahihi na iliyochambuliwa na wataalamu wahabari nakupitishwa kuwa moja ya habari bora zilizochaguliwa kusomwa na mtaalamu wa kusoma habari. Baada ya taarifa ya habari kunakua na matangazo ambayo yanaletwa kwenye runinga na redio ili kuwajuza watu kuwa kipi kimeundwa na wataalamu ili kiweze kutangazwa na kuweza kuheshimika na lengo ni  kiwafikie wasikilizaji na watazamaji walio wengi.
Pale mtu anapoamua kufanya kitu ujue kwamba alishakifikiria, hivyo anataka afanye kitu kilicho bora na kuweza kuvuna na kujivunia  kilivyo bora, mtazame mkulima anaanza kwa kutayarisha shamba, baadae anapanda na baadaye kuvuna, na kwa kipindi chote hicho amekua analitazama na kulilinda shamba lake kwa umakini mkubwa sana, huwa anaitwa mkulima kwakua anaelewa nyakati za kufanya ukulima wake, yeye ni mtaalamu wa kulima ndio maana anaitwa mkulima, pia ni mtu huyu anayeheshimika kwasababu anaheshimu taaluma yake, kwasababu anayeheshimu sana shamba lake, jembe pamoja na mbegu. Huwezi kukuta mkulima anacheza na jembe wakati wa kulima, au anachezea mbegu wakati wakupanda, huwezi labda kama sio mkulima,  ila kama wewe ni mkulima basi utaheshimu ukulima wako.
Kwa hiyo kama wewe ni mwanafunzi, daktari, mwalimu, mfanyabiashara, mwanamuziki, mwanasiasa au mtu mwenye utaalamu fulani lazima uheshimu utaalamu wako na ufanye jitihada kusoma nyakati ili usije ukapotea katika dira ya utaalamu wako. Unapoona ama kusikia mtu anaitwa mataalamu ujue ni zaidi ya jina na ni mtu mwenye elimu, ustadi au ujuzi  wa fani au jambo fulani maalumu , mwenye malengo na upendo na utaalamu wake.
Kiukweli dunia ya sasa imebadilika, imekua dunia ya wataalamu na mwenye utaalamu ndiye anayepewa kipaumbele katika mipango iliyo endelevu. Itafika kipindi watu tutakua tunaaminiana sana kutokana na kila mtu amekua mataalamu wa jambo fulani, inafika kipindi kunakua na sehemu maalumu ya kuwakuta vijana wa Kitanzania wakiwa wanajadiliana kitaalamu kua tunataka tufanye jambo la kimaendeleo ili kuliletea Taifa letu maendeleo kwa heshima zaidi ya jina.
Hii inawezekana kama vijana wa kitanzania tukiamua kuheshimu hisia zetu, wewe kama kijana unataka uwe nani hapo baadae? Baada ya hapo uiheshimu mipango yako, “kwasababu tukiamua kwamba tunaweza kisha tukajifikiria kwamba tutaweza  basi tumeweza”.  Vijana wengi tunashindwa kutimiza malengo yetu kwasababu hatuheshimu mipango na malengo yetu, wengi wetu tunajikuta tunaishia katika fani ambazo sio zetu, hivyo tunazidi kulipotosha taifa letu kwa utaalamu usio katika fani na ndoto zetu alimradi tusife njaa.
Siku zote ukitaka kufanikisha na kufanya kitu kikawa kizuri, basi kifanye wewe mwenyewe kwa moyo wako na kwakupendo wako toka moyoni mwako, ni vizuri tukaheshimu hisia zetu kwa kufanya kazi tulizoziota tokea utotoni. Tusiishie kukimbilia bora fani ila tupiganie kupate fani bora
Pia sisi kama vijana kama tunataka kuwa watu hapo baadae, yatupasa  tuheshimu taaluma zetu ili tuje kua wataalamu wa fani mbalimbali, tusiwe watu wakutizama  upeo wa macho na pua bali  tutazame mbele wapi tunaenda na wapi tuna taka kufika, ni malengo gani tumejiwekea, pia tusiwe wataalamu bora kwakuongea sana bali wataalamu bora kwakutenda kwa vitendo. Najua ni vingi vinahitaji mabadiliko ila anza kwa kujibadilisha wewe mwenyewe, angalia nini kinachohitaji mabadiliko ndani ya moyo na fikra zako, tusiwe watu wa kuacha mambo yaende kama yalivyo, bali watu wakubadilisha mambo yaende kama tulivyo na namna tunavyotaka yaende, tusiendeshwe wakati tunaweza kuendesha,  tutasubiria mapaka lini mkombozi arudi, wakati wakombozi ndio sisi wenyewe na nafsi zetu. Kijana "kujikomboa kifkra na kiroho, ndio ukombozi wa mkombozi aliyesema atarudi". kijana wa leo jitazame zaidi ya jina kwamba wewe ni nani? vipi heshima iko pamoja na wewe? unaheshimu taaluma yako? Je wewe ni zaidi ya wanavyokutazama? nakusihi kijana mwenzangu kwamba kutafuta taaluma ndio heshima ya kwanza, jina litakuja wakikuhitaji. Watakuita tu....ULAMAA KUNA KAZi TUNATAKA UiFANYE..!Kumbuka kwamba kumkichwa ni wewe!

Thursday, October 21, 2010

Wednesday, October 20, 2010

KUMKiCHWA CLUB

JE! UNAiJUA kumkichwa.blogspot.com.WAKATi WA MAPiNDUZi SASA UMEWADiA.TUMUOMBE MUNGU ATATUSAiDiA.......kumkichwa.....