Saturday, May 28, 2011

"DUNiA UNAYOiTENGENEZA"



Wahenga walisema utaicheza ngoma kadiri utakaisikia midundo yake, na hii inadhihirisha kwamba mdundo utakaposimama basi yakubidi kusimama. Dunia tunayoitengeneza ndio Dunia tutakayoishi. Ukiutazama mfumo wa maisha tunayoishi ni mfumo ambao tunautengeneza sisi wenyewe kwa maaumuzi yetu kisha tunaufuata mfumo huo kama unavyotutaka tuufate. Matakwa yetu ndio yanayotufanya tuunde mifumo hii ya maisha, kisha ili kutimiza matwaka yetu inatupasa kuufata mfumo tuliouunda.

Dunia imekua kama ngoma tunayoiunda sisi wenyewe kisha tunaanza kuicheza kufuatana na midundo yake. Kuna midundo mbalimbali inayotoka katika ngoma hii tuliyoitengeneza, ambayo inatubidi tuifate wenyewe, na baadhi ya midundo ni lazima uifate sio hiari yako, kuifata ni lazima ili uendane na wenzako walio katika mfumo.

Katika sayansi na teknolojia tunazoziunda kila siku, tunajikuta tunaunda na kuvumbua aina mbalimbali za mashine na taaluma mpya kila kukicha. Kwa mafano nguvu za nyuklia ni moja ya matokeo ya sayansi na teknolojia ya wanadamu katika ugunduzi, lakini gharama za kuitunza na athari zake ni kubwa mno. Hivyo walipounda ngoma hii ikawabidi waicheze kama inavyotoa midundo yake. Juzi juzi tumeshuhudia tetemeko la ardhi lililotokea baharini huko Japani na kusababisha vinu vya nyuklia kulipuka, ikawabidi wajapani kuicheza ngoma kama walivyoisikia midundo yake. Hii ni hali halisi inayodhihirisha namna dunia tutakayoiunda ndio tutakayoifuata kama inavyotutaka twende.

Katika mfumo wa maisha, binadamu alijikuta anaunda fedha kama njia ya kubadilisha bidhaa ama kitu chenye thamani. Ila katika njia hizo binadamu hujikuta katika wakati mgumu katika kuzitafuta fedha hizo. Ila kwa kua binadamu huyo huyo ndiye aliyeunda ngoma inayotoa mdundo wa fedha, inambidi acheze kwa mdundo wa fedha, yakupasa kuamka kila siku asubuhi, ukizifikiria pesa, yakupasa kulala usiku ikizifikiria pesa, fedha imekua ngoma isiyosha masikioni mwa binadamu, yampasa kuicheza kila mdundo wake inaposikika kwa kua ndio dunia aliyoitengeneza mwenyewe. Ukicheza tofauti na mdundo utajikuta uko nje ya mfumo na huo ndo mwanzo wa kuunda mfumo mwingine ambao nao utabidi uucheze kama unavyodunda ili kuufuata mdundo.

Katika siasa nako kumekua na midundo mbalimbali mfano wa demokrasia ni mdundo ambao unachezwa na jamii nyingi duniani kwakua eti ndio unoleta usawa katika nyanja ya siasa. Kuna modundo ya kubepari, kijamaa, kifalme, kitwana, kitumwa na mingine mingi. Kwa mdundo mtakaouchagua ndio mdundo matakoufata. Kwa mfano walio katika mfumo wa kifalme yawabidi kuzicheza ngoma za kifalme, kwa walio katika mfumo wa kawaida kwa kumchagua kiongozi wao wenyewe, nao watacheza ngoma yao wenyewe, kama watamchagua kiongozi mbaya itawabidi kufuta midundo yake, wakipata kiongozi mzuri basi na midundo yake itakua mizuri na watamchagua tena. Kwa hiyo yatupasa kua makini wakati wakufanya maamuzi makubwa kama haya wakati wa kuwachagua viongozi wetu kwakua tunaiunda ngoma tutakayicheza kama inavyotaka.

Katika mfumo muhimu kuliko yote ni elimu. Mfumo huu ukekua mzuri sana kutokana na namna unavyorembwa na maneno matamu kama “ELiMU Ni UFUNGUO WA MAiSHA/MAFANiKiO”, “ELiMUNi MWANGA”, “ELiMU Ni BAHARi”, waliyoyaweka maneno haya wanajua utamu wa elimu upo wapi, pia wanatambua kua kuna misukosuko inayomtokea yule mtafutaji elimu, na ndio maana wakaweka maneno matamu kama haya ili watafutaji wa elimu wasikate tama mapema, kwani ukiipata elimu vizuri basi utamu wa elimu hiyo utakuchezesha ngoma uliyitengeneza mwenyewe, kama uliunda ngoma yako vibaya basi na mdundo wake utakua mbaya kama ulivyouunda. Ila ikumbukwe kwamba unapotegemea matokeo mazuri uje uko kwenye hali mbaya, unapochumia juani basi utalia kivulini, machungu na matamu ya elimu anayajua yule mtafutaji asiyekata tamaa ya kutafuta elimu. Utamu wake haupo tu katika kupata mafanikio, bali kua na uwezo wa kuelewa mambo kwa urahisi na kutambua ukweli wa dunia na midundo yake. Ukiwa na elimu Nzuri unaweza kutengeneza mfumo mzuri wa maisha ambao utaweza kucheza kwa kufuata midundo yake bila wasiwasi wa vikwazo vyovyote.

Kwa ujumla mambo tunayoyafanya kila siku yanaunda kesho yetu, utakachokifanya leo kesho kitaleta matokeo yake, sasa yategemea matokeo yake utayakubali ama utayakimbia, utakapoyafata utakua umecheza kufuatana na mdumdo wake, pia kama ukikimbia matokeo yake utakua unaunda ngoma nyingine ambayo nayo itakubidi uifuate midundo yake ya kukimbia. Jambo la muhimu ni kuwa makini wakati wa kuangalia aina ya ngoma unayoitengeneza, midundo mingine ni migumu katika kuifata, yatupasa kuicheza huku mioyo ikilalamika. Kwa mfumo wa maisha ya sasa wengi wanalalamika ila ndio ngoma mlioitengeneza kwa ubora mlioahidiwa, kwa kipindi kinachuguja tuwe makini wakati wa kuchagua ngoma ya kucheza kwakua Ngoma tunayoitengeneza wenyewe tutaicheza kama inavyotaka kwa midundo yake, na ngoma hii ni Dunia tunayoitengeneze kila siku. Tambua kwamba KumKichwa ni WeWe.
Kajiabeid©2011

"MUDA GANi?"



1.Utasimama kama mwenye haki anayedai chake kwa haki?

2.Utakaoacha kulalamika wakati nguvu akili viko ndani yako?

3.Utatambua ulivyo ni matokeo ya vitu na mambo uliyoyafanya kwa muda uliopita na ndio yanayokufanya uwe hapo ulipo katika muda huu na ni kwa namna gani unatakiwa ufanye mambo kwa muda ingawa haujui ni kwa muda gani.

4.Utakubali kuwa wewe ili uendane na muda wako uliopewa kukamilisha na kufanikisha wajibu wako.

5.Utakao kua chini ukifikiria kupanda juu na muda gani utakua juu na utakumbuka kwa muda gani ulikua chini ili muda wakua juu ukiisha usirudi chini kwa muda usioujua.

6.Utathamini kila kiumbe kilichokujia kwa muda kukamilisha ukurasa wa kitabu chake na chako bila kuwakwaza kwa kutotambua muda gani aliyekuumba atakileta kwako hicho kiumbe.

7.Utakaothamini muda na kwenda nao sambamba bila kupoteza dakika moja yenye uzito wa sekunde sitini.

8.Utakua umejiaandaa kuondoka katika dunia hii na kutarajia mema kwa wema uliyofanya na mabaya kwa baya uliloyafaya.

9.Utakao tambua kwamba maisha ni mtihani unao ufanya kila siku bila ya wewe kujua.

10.Utathamini ulichonacho na kuacha kutumbulia mimacho cha mwenzako kisicho chako.

11.Utagundua kuwa muda gani ni muda huu unaoutumia kufikiria ni muda gani utatenda vilivyo ndani ya Muda gani na kwa muda gani? Kumkichwa ni wewe!

Kajiabeid©2011

"Kwa Walio Juu na Chini"



Utamu wa Maisha hujitokeza kwakua kuna misukosuko inayotufanya tujitambue kwa mapana na marefu. Mfano wa misukosuko hiyo ni juu na chini, yaani leo uko chini na kesho upo juu,leo umepata kesho umekosa, leo kipo kwako kesho kwa mwenzako. Kamzunguko kanakoashiria uhalisia kwamba mamlaka yakupanga hayapo mikononi mwako. Tazama uhalisia wa usiku na mchana,vinapo pokezana ikifika Asubuhi Jua linachomoza kisha tunapata mwanga wake na ikifika Jioni giza linaingia na tupata mwanga hafifu wa Mwezi kuashiria hauwezi kukosa vyote. Kwenye giza la Usiku unapata mwanga toka kwenye Jua kuashiria urafiki bila chuki. Na ndivyo ilivyo kwenye maisha yetu haya ya kila siku kwa wenye urafiki bila chuki.

Ukikubali kuna kusini pia ukubali uwepo wa kaskazini, iweje utambue uwepo wa mashariki lakini hutaki kutambua uwepo wa magharibi. Jambo la muhimu na la msingi ni kukubali uhalisia katika maisha yako, kama umeona jua linachomoza leo, jitahidi na kesho ulione, ukiliona wakati linazama usihuzunike kwani kuzama kwake leo ndio kuchomoza kwake kesho.

Mwanzo ni mwisho na mwisho ni mwanzo wa mwisho mwingine. Hii ni hesabu ndogo hata mtoto mdogo anaweza kuielewa na kuijibu, kusingekuwepo na giza tusingekua na mwanga mwingi. Kama hakuna giza basi na mwanga usingekuwepo, sababu giza linategemea uwepo wa mwanga, kama maisha na kifo vinavyotegemeana ndio hivyo ilivyo kwa walio juu na walio chini wanavyotegemena.

Aliye juu sikuzote hatamani kwenda chini, na sio kwa mapenzi yake yaliyomfanya awe juu bali mamlaka ya aliyetuumba. Aliye chini ndoto zake ni lini atafika juu, huwa anatamani nae afike juu siku moja. Kiuhalisia ukitazama hakuna anayependa kudhalilika, ingawa kudhalilika kunaendana na kuheshimika. Aliyechini anaona aliye juu anaheshimika, na aliyejuu anaona aliyechini anadhalilika ndio maana hatamani kurudi chini. Ni kweli binadamu haturidhiki na tulivyonavyo, aliye chini anaona hana kitu kwa kujifananisha na aliye juu, aliye juu naye anatamani uhuru wa aliye chini. Hakuna anayetambua fikra za upande wapili wa jani kwamba kuna matatizo.

Milango yote inapofungwa hua kuna milango mingine inafunguliwa katika upeo wa macho na fikra zako, ieleweke milango ni nafasi ya kufanya au kuchukua hatua nyingine tofauti na ile ya ya kwanza ambayo imefungwa, mlango wa kwanza utakoupata uko wazi, wapili ule unaotakiwa ufanye juhudi kuufungua, mingine ni ile utakayoifungua kwa kusaidiwa na watu uliowategemea au usiowategemea, uamuzi ni wako. Tambua uwepo wa njaa na shibe, hata uwe na njaa ya siku sita utakua mlo mara moja tu, kisha utasikia njaa tena baadae, mgawanyiko wa viwili unaosababisha uwili kwa mtu mmoja. Ila utakavyo amua ndivyo fikra zako zitapokupeleka, ukiamua kutafua bila kukata tamaa utapata, kwakua vikwazo vipo kila mahali, unapokitaka kitu ili kuwa nacho lazima ukifahamau kwa undani, mafunzo hayo yanaweza kukujenga ama kukubomoa. Tambua kwamba Waroma hawakuijenga Roma kwa siku moja, ila aliye chini anataka akiamka asubuhi ajikute yuko juu, laa sio hivyo wewe uliye chini, lazima upambane kwanza ndipo atakapo ijenga Roma yako, kwani aliye juu naye ataendelee kuimarisha Roma yake.

Hivyo kwa tuliochini tutafika juu siku moja, na kwa walio juu wanatambua kua ipo siku watashuka chini, ila tusiwasubiri washuke na wala tusiwaombee washuke, sisi tupamabane ili tuondokane na firka za chini, tupiganie kilicho chetu kwa haki, tuvune kilicho jasho letu, kwani ukikubali kuonewa ni sawa na umetenda dhambi. Kwa hiyo tuwafate huko walipo, kama unataka kubaki chini endelea kubaki, lakini kama unataka kwenda juu, unatakiwa ujipange leo, utazama mbele, uweke malengo, kisha uyatekeleze, usiyapuuze na wala usikate tamaa panapo ushindi panapotokea na matatizo vikwazo, kwani matatizo na vikwazo ni sehemu ya mchezo. Inapokua ngumu wewe kua mgumu, jitambue wewe ni nyundo mbele ya jiwe, ligonge tena na tena mpaka livunjike. Lakini zaidi ya yote kumbuka kumkichwa ni wewe!

Abeid kajia ©2011

Friday, May 13, 2011

A SMiLE THAT CHANGED MY LiFE

...A smile that changed my LIFE..by Glicious


                      A friend had once asked me about what I wasn’t comfortable with when it came to my body and God only knows the list I came up with... I was like I don’t like this and that and that. The only things I kept were my eyes, my nose and my face in an overall. Why did I choose to keep these three as they were? It’s because I have memories that I wanted to cherish. I have been told and I actually believe I got my eyes from my dad and I look like my mom that much I know. I would keep them for they are my parent’s replicas. However, I recently went to visit my grandfather and I realized how wrong I was. The first thing I voted as something I would have liked to change was my smile (my teeth in particular), my forehead, my pimples and my long chin (I don’t believe its that long but that’s what I have been told so I would say I learnt to believe it)

              I would call my trip revolutionary! It was just one day spent with my old man but I learned a lot about him and more so about myself, I looked at him as he talked, observed every gesture he made, every facial expression and every wrinkle he had and I remember thinking that he was the most handsome old man I have ever known! I remember thinking that even George Clooney wouldn’t look so good when he is 84 years old! That’s when the magic happened…he smiled..With a smile which awakened happiness and warmth in my heart. And with no objection I smiled back to what then struck me as a very familiar gesture. I could remember I wished he does not stop smiling to me. That’s when it hit me! The smile that had awakened the warmth, relaxation and serene in me was familiar to me because I had spent generous amount of minutes criticizing. It in front of my bedroom mirror, I had been shallow by spending time thinking of ways to perfect it or stop it from showing or seen if it could not be perfected instead of concentrating on the message it is supposed to send, that of love, happiness and acceptance.

My friend called me stupid and crazy after I had listed down all the “defective” features and I came to realize from my trip that he was right.

                  My chin might be extra centimeters longer than the rest, my teeth a bit bent and my forehead a bit protruding, so what? What are teeth for? What is a forehead for? What is a chin for? They might not be fit to showcase but they sure do what they are supposed to. My chin was passed down through the genes of my dad and thus they stand for what my bloodline is...it is a mark of my origin and I hold my family line very dear to me. Then is it reasonable to want it changed? Can one change his bloodline? That is unthinkable!! As for my forehead, isn’t it from my dear mom? It definitely is. Have I had enough sentimental reminders from my parents? I don’t think so! Plus whatever material thing I have that reminds me of them will eventually perish but this face, this body physique will only perish with me. This face and body is the only thing that reminds of my past and with them I will create my future.

"A Mirror"

A Mirror


          The reason they say that variety is the spice of life is, as a human being there is a time you should let yourself go and experience the wonders of the world to make your life more exciting. Perhaps I can say we came from different families and from this we have various qualities and bitterness of life which make us behave differently from each other. The way we behave towards others is kind of hard to realize that it reveals our strength and weaknesses when problems find us. That is why it comes a time when the apple must roll far from the tree to discover the beauty and worst of the world, and from there we might discover things we never experience in our lives or in our families.
         As the time approaches, you must break the back of anything, there you must also interact with people in the outside world, make friendship with other people, and the way you interact, and you tend to learn different things from them. Things like their weakness and their strength, also they usually learn different things from you, and I discovered that one man’s meat can be another man’s poison, your strength can be your friend’s weaknesses ‘mutatis mutandis’, there you will learn new skills. And that is one of importance why we must interact with outside world.
              William James said that “the greatest discovery of my generation is that a human being can alter his life by altering his attitudes of minds” the way we think is the way we will behave and in order to learn new ways of life that our partners experienced in their life time we must first change our attitudes toward them. There are things in life you learn logically and others emotionally, because from our families we learn how to be logical from male and emotional in female. One thing I have lean in life, in order to live with integrity is to allow the interaction with others with an optimistic attitude, though it is not always bad to behave in pessimistic attitude, but my friends it’s better to be optimistic toward your friends than being pessimistic and a positive attitude towards friends will help you when your friendship faces twist and turns or ups and downs. Remember what Mickey Rooney quote that we have to learn new different things in our life from different sources because life would not be fun if it did not have its ups and downs.
            According to my research I discovered that there are two things which make us in needs of friends, It can be our inner common interest and our inner problems or our outside challenges, thus what happens when we lose interest and when our problems had been solved is that we tend to lose contact with our friends, but one day or night when troubles find us we contact those people whom we think they can give as a hand to solve our problems.
            At one time love also can unite us with those we love and those who  love us, but for some time love is there and other time it’s not there, there you will experience a new feeling which will make you in quest for new solution, there you meet new friends. So love is something which for sometimes is here and sometime is not there.
           For my knowledge what goes around will always comes around, which means there is something which reflect what you are doing, and as it comes around you the one who will experience it, while you are in the center point of my mirror, means that you will always see yourself in the mirror, because this mirror reflect what you are doing, when things go wrong the mirror will reflect the same, when you do good things the same will be in the mirror.
         The point is the relationship is a mirror, whenever you are related with a person, a friend, a lover or an enemy a mirror is there, it reflect what we are doing, that is why when we look for friends we base on two things; common interest and inner problems to those we think that they can help us to solve them, also a friend must be someone who is  never afraid to criticize you when doing something on either ways, but there stupid people who see their face in the mirror and they see it ugly they destroy the mirror, the mirror does not make you ugly and by destroying the mirror you do not become beautiful, if you see ugly friend don’t try to leave your friend, the ugliness is in you, just drop the ugliness in you and this mirror will reflect a  beautiful image, and be thankful for this mirror, and remember the closer the relationship the clearer is the image on the mirror. A friend must be a person who never pulls you down, when we behave bad the reflection on the mirror must tell the same and a good friend will never smell a rat on anything you say, though some of friends are like snakes in the grass never afraid to let you be in queer street, you must be extra carefully or it’s better to stay alone than to pin one’s faith on a friend with bad faith.
          An enemy is a friend on the opposite direction so never afraid having enemies, your friend may be afraid showing your weakness but your enemies may use your weakness and with the help of self discovery to strengthen your weakness. The enmity has its own beauty, it a sort of friendship on opposite pole, it is love affair on the opposite direction. I quoted Osho in his book “Meditation the Ultimate Adventure”, that “if you have loved friends, you will love your enemies, because once you know the beauty of friendship, you also come to know the beauty of enmity, is a friendship in a reverse order”. Kumkichwa ni wewe!
Kajiabeid©2011

Sunday, May 8, 2011

"MAPiNDUZi YA KWANZA Ni KUUSHiNDA UOGA NA UBiNAFSi"

   
          Kwa kipindi kirefu tumejikuta tumekua ni watu wa kuongea sana kuliko kutenda. Kila mmoja miongoni mwetu amekua na fikra za uyeye na familia yake huku tukisahau umuhimu wa kuwa na jamii pamoja nasi. Tumesahau kua yule anazalisha kile ili na sisi tukizalisha hiki twende sawa. Ubinafsi wa nafsi umetuingia katika fikra zetu na kutunyima mwanya wakufikiria yajayo kwa taifa la kesho la wajukuu zetu, na hili limechangiwa kwa kiasi kikubwa na uoga uliopo katika nafsi zetu, kumbuka hatuwezi kuongelea taifa letu la kesho kama hatutalijenga leo, na kwa mapinduzi ya uoga ndani ya nafsi zetu utakua ni ushindi mkubwa sana kama baina yetu tutalitilia maanani suala hili.

              Uoga ni hali ya kuhisi kwamba uko kwenye hali ya hatari au jambo lolote baya linaweza kukutokea, au hali ya hatari itatokea wakati wowote. Uoga huu upo miongoni mwetu hasa pale tunapofikiria kufanya mabadiliko kwenye mfumo wetu wa maisha. Ndio maana wataalamu wanawaita watu walio katika kundi hili wahasi (mtizamo mbaya), kundi lilopoteza matumaini ya kuzishinda nafsi zao mbele ya vikwazo vinavyowarudisha nyuma.
              Nikimnukuu mwanahistoria mmoja alisema" katika ugunduzi mkubwa wa binadamu ni kwamba binadamu anaweza kubadili maisha yake kama ataweza kubadili fikra zake", alisisitiza kubadili fikra kwakua ndizo zinazompelekea mwanadamu kufanya kitakachomjia katika fikra zake. Kama fikra zitakua za uoga, basi mtu huyu atajiona yuko kwenye hatari hata kama hakuna hatari yoyote inayomkabili. Kuna usemi unaosema uking'atwa na nyoka hata ukiguswa na ujani basi utadhani ni nyoka, hii inatokana na kuwa na fikra za uoga, kama wewe ni jasiri pambana na nyoka huyo, pia kama hakuna nyoka ya nini kuogopa jani.
             Jambo la muhimu na la msingi ni kusimama imara kwa fikra zenye matumaini katika kila jambo pasipokua na uoga. Ni dhahiri binadamu tumekua na hulka ya kujisaliti wenyewe kabla hatujasalitiwa, na hii inadhihirisha pale tunapoamua kulala wakati jua linachomoza, tunapofurahia mkulima anapokula mbegu, tunapojadili kila siku ni nani wakumfunga paka kengele, tunapolaumiana kwa kunyoosheana vidole kwamba yule kafanya vile huyu kafanya hivi, tunaposhangilia mtoto wa jirani yetu anapoanguka anapojaribu kutembea wakati mtoto wako angali bado yupo tumboni mwa mama yake.
              Ningependa kuwasisitiza sana vijana wenzangu kwamba mapambano bado yanaendelea, uwe umeyaona ama hujayaona, na maisha yenyewe ni mapambano tosha, na kwa ubinafsi na uoga tulionao, hatutafika popote, tutazunguka na kurudi pale pale tulipotoa. Mabadiliko yanahitajika miongoni mwetu katika jamii zetu, mapinduzi ya kuushinda uoga katika nafsi sio madogo, ingawa  hayahitaji kushika mtutu, bali kukaa na kuangalia ulipotoka ni wapi na ni wapi unapotaka ufike. Kuna mbinu mbalimbali za kushinda, ila kwakua ubinafsi na uoga ndio vimetutawala, yatupasa tuanze na nafsi zetu kwanza kwa kuondoa fundo la mchanga lililo machoni mwetu, kisha ndipo tumtazame jirani yetu tumtoe kakijiti kalicho jichoni mwake. Mapinduzi haya yanaanza kwako wewe mwenyewe, kisha yatasambaa yenyewe kama yatakua ni yenye harufu nzuri, ila ukishindwa usinilaumu mimi kwakua mapinduzi haya yanaanza na wewe. Ndio maana tunasema Kumkichwa ni WeWe!  


kajiabeid(c)2011

Wednesday, May 4, 2011

"The other side of the leaf"

Lake Jipe

Aerial

Sacred Tree

Lord Give me a SiGN

The Road to no where

Car Parking

home sweet home

 Maisha bora

Pare Mountains

Pare Mountains

The Late Grand House

Kumkichwa

Msonge House