Thursday, September 27, 2012

Ebwana daah John Blass Hii Ni M.A.S.S.I.V.E




Feels good to be back,back with old friends,back to what I love doin,,,special thanx to Cannibal Shattah,JCB Jcb Makalla, Mike David, Nakaaya Sumari, GNako warawara, Niki wa pili, Mo Plus, George Sengati, Thai Tha 1, Tricky D.T and Skinny Ma'Role for making this happen..love ya all....

                         
                            Facebook Comments about Wazi

Ebwana eeeh daah John Blass Grand ameuaaaa R chuga Stand Up am the 1st 1 kusikiliza ngoma Ya WAZI ni juu juu tu lkn inadatisha stay tune maraia lzm mdateee .......loading...96%
— with 

  • Gasper Mbasha the count down begins homy

    Lexa Julius braaa R chuga inatega dis world soon sa hiv ni level za kimataifa not kitaifaaa yereeeeeeeeeeee

    Lexa Julius Stay Tune Gasper mtadata

    Obe de Honest Waazi!haina maxwali joh,raizin to the top

    Lexa Julius Stinyoo hii ngoma ni nyokooo umesoma kwanza hizo vichwa vya R ni best n ever collabo broo

    Obe de Honest Nmexoma arif ni combination moja deadly cana,unyo tayari ama

    Lexa Julius Soon on air braa

    Jackson Kway hiyo WAZI si itakuja na show pia ama? @ lexus julius

    Lexa Julius makila kitu boob




Huyu Ndiye Thai aka Tha 1 Artist Bio & Video collabo na Tz Artists(Coming Soon)

 Huyu Ndiye Thai aka Tha 1 atakayekua kwenye wimbo wa Wazi ambao utakua na wasanii wengine kama JCB, Cannibal,Mo Plus, Nakaaya, G Nako, Niki wa Pili, Bonta, Joes(North Dwellers), Tricky D.T toka South Africa na Slim Deezy(North Dwellers)



Click here to review the Biography

Wednesday, September 26, 2012

100 THOUSAND POETS FOR CHANGE



Arusha Poetry Club with LA POETISTA OPEN MIC based in DAR ES SALAAM hosting the event 100 thousand poets for change in TANZANA,100 THOUSAND POETS is POETRY MOVEMENT all across the world ...dont miss it in ARUSHA at the same date that will be happenin all over the world..karibuni

 This will be a special ARUSHA POETRY CLUB Edition #3!! We will be hosting the world wide event 100 THOUSAND POETS FOR CHANGE on September 29 at the place where art happens...Masai Cafe! Bring your poem and bring your ears! We are indeed poets for positive social change both in our country and around the globe. PLUS there will be a special gathering of musicians who will use indigenous instruments and vocals to bring poetic visions to life through music!! The excitement is building!! Be there A.town!! Support the ARTS! Support POETRY!! Be there or you know what...be square!! by Charlotte Hill O'Neal

Facebook Comments about 
                    100 THOUSAND POETS FOR CHANGE
  • Neva E. Wartell Wow, this is great! I'm sharing with all my poet people...

  • Diane Strong I guess Kyomushula will be one of those 100 thousand...:)

  • Raphael Mukimala Kato Bitungwa damn i wish i could make it

    George Kyomushula @Neva thats ryt..thankx alot,spread the world

    @dada Diane APC got almost 149 people,without a doubt hundred of them are poets,and not less than 20poets attend each edition..i believe Arusha will donate 50poets into ONE HUNDRED THOUSAND POETS FOR CHANGE,WORLD MOVEMENT..

    @Raph bro send A person to represent you
  • Young Ticha im in and I will donate my poems too George

    George Kyomushula ths time come early,dont come up with kriss kross excuses I MISS THE BUS..lol

    Young Ticha hahaha.I won't

    Jcb Makalla nitakuwepo kwenye hii...g sore kwa leo inabidi uielewe mitaa..tupange kesho..

    George Kyomushula Jei poa poa nipo HARDWARE mpaka kesho..so utanishtua au vp?leo mitaa niliielewa..lol

    Peter Arsenal Mboye Kama kawa i will be there

    Shubira Bocko One of these years; I'll make it to the Arusha poetry club. I'm slip through with an Erikah Badu hair wrap, Queen size earrings, and do some black consciousness spoken word...LOL All jokes aside you all have a great time keep on inspiring;Tupopamoja in spirit!

    George Kyomushula @Mboye usikose,njoo uue

    @Shushu u got jokes,i wl b happy to c u on stage
 

"MZIGO WA LAWAMA"




Ni wewe! Sio mimi! Kama sio wewe ni yeye! Sio sisi ni wao!  ni baadhi ya kauli za mkwepaji na wakwepaji wa lawama, hakuna anayependa kuubeba mzigo wake hata kama ni wa uzito wake, hata kama ameujaza mwenyewe. Katika kitabu kitakatifu cha biblia kuna mstari unasema"kila mtu atabeba msalaba wake" na katika kitabu kitakatifu cha Quran kinasema "hata kama ni mdogo mithili ya mdudu sisiminzi ni wakwako utapimwa na utapata malipo yako kwa ujazo wake". Ila je uko tayari kuubeba mzigo huu?

Binadamu huwa tuna hulka ya kukataa uhalisia, ila kwakua kuna ukweli ambao hauwezi kua uongo na uongo ambao hauwezi kua ukweli, basi tujue kuwa tutaubeba tu. Tazama Mfano huu
      "Mbegu ya mti inawekwa kwenye udongo wenye rutuba, kisha inawekewa mbolea ili ikue na ichanue na ili uwe mti bora na wenye afya inabidi utunzwe kwa makini, kama ni mti wa matunda basi utoe matunda bora na kama ni wa kivuli au mbao basi uweze kukidhi mahitaji ya aliyeweka mbegu ile. Mti huu utakutana na dhahma mbalimbali kama vile mvua, upepo, jua, moto hata kufikia kukatwa na watumiaji kwa matumizi yao".

Ila je unatambua kua wakati wa mvua mti huu huvumila sio kwakua hauna mahali pakujikinga bali umekubaliana na hali halisi, iwe mvua liwe ni jua kali mti huu utavumilia, upepo mkali utapita na hata kama moto utatokea mti huu utabaki palepale. Sasa nikuulize wewe, ninyi na wao Je!  uko/mko tayari kubeba lawama za mti kama mti ukitaka kulalamika? Jiulize kama mti ungekata tamaa kwa changamoto mbalimbali katika ukuaji wake Leo ungepata matunda yaliyo bora kutoka katika mti bora? Je Leo ungepata kivuli? Leo ungejivunia mbao za mninga?

Kilichopangwa kutokea hutokea, kilichotakiwa kufanyika hufanyika, palipokosewa hurekebishwa, tunajifunza kwa makosa, tunakuzwa kwa mafunzo, tunafunzwa na matatizo. Mzigo wa Leo ni bora kuliko wa Kesho, uzito wa Jana ni mwepesi kuliko wa Leo, wa Leo ni mzito kwakua upo nao Leo. Huwa tunadhani kwamba matatizo ndiyo yanyotunyima kuchanua na kusahau ya kua jua, mvua na upepo ndivyo vinavyosaidia katika uchavushaji na ukuaji.

Kiukweli palipo na uchanya uhasi lazima uwepo, palipo na ubaya pana uzuri, hizi fikra za kweli palipo na ukweli. Tambua pale unapolalama kwa uhasi unajinyima nafasi na wakati mzuri wa kutafakari uchanya wa mambo. Mfano kama mti ungekua unalalama na kutoa visingizio, je ni nani angekubali kubeba lawama zake?

Jiulize pale unapokosea au unapokosewa kuna umuhimu wa kumbebesha mtu lawama? Mimi nadhani cha muhimu ni kutazama palipokosewa kisha kujifunza na kurekebisha kosa hilo kwa pamoja. Tusipoteze muda wa kutafakari nini kifanyike kwa kung'ang'ania kumtafuta mtu wakumbebesha lawama. Kinyume na hapo basi sintopenda niubebe mzigo huu wa lawama kwakua Kumkichwa ni wewe!

Tuesday, September 25, 2012

Islamic Help Worldwide Shelter and Infrastructure Projects


Can you imagine not having a roof over your head? For many hundreds of thousands of people, this is a reality. Islamic Help aim to provide housing for thousands of people who currently live without a house. From our housing complex in Pakistan, to our Eco-Village for orphans in Tanzania, many people can sleep well thanks to your help. Out work also includes providing community hubs such as mosques for communities to rally around.

Monday, September 24, 2012

Beti na Mdundo

Jcb ft. Niga-BWiii BRAND NEW kutoka WATENGWA RECS


BRAND NEW kutoka WATENGWA RECS.......DOWNLOAD FOR PROMO....
ikiwa imetengenezwa na Daz Naledge na kufanyia mastering na Ambross a.k.a Dunga wa Mandugu Digital...
Hii hapa kazi yenyewe baada ya kazi kubwaa
BWI----Jcb ft. Niga (Mtoto wa Bibi)




"Chini ya Jua Nimeweza"



Maswali mengi yaliibuka,yameibuka na mengine yataibuka, kivipi ameweza?..ila jibu ni moja tu..kumkichwa ni wewe!

Hakuna asiyeweza, hata asiyeweza anaweza kwa kukubali kua hawezi. Maisha ni safari na safari yoyote huanza kwa hatua, je uko tayari kupiga hatua ya kwanza? je umeshapiga hatua ya kwanza? Je umeangalia umbali wa unapoelekea au umbali wa ulipotoka?..

Umakini ni kitu cha muhimu sana ila upendo ni kitu kizuri zaidi. Je unapenda unachokifanya kwa umakini? je unafanya kwa umakini unachokipenda?. Jana inatofauti na leo na leo sio sawa na kesho, muda unatuacha, muda uko makini, muda haupotezi muda, je muda wako unautumia kwa umakini?.

Tumeumbwa kisha nasi tukaunda, tunaunda kwakua tumeumbwa na akili, tumepewa uwezo wa kufikiria ndani na nje ya sanduku. Kilicho nusu kinaweza kua kimejaa nusu au kimepungua nusu. Uamuzi ni wa fikra zako kwa macho na masikio yako.

Unaamini au unajiamini ni juu ya imani yako, je unaweza, umeweza au utaweza?hiyo ni siri yako ndani yako juu ya uwezo wako na mapungufu yako. Hakuna kinachoshindikana chini ya jua. Visingizio na lawama havina tija zaidi ni hasara na kupoteza uaminifu juu yako. Unapoaminiwa kisha ukavunja uaminifu haimaanishi aliyekuamini ni mjinga kwa kukuamini, bali amekupa kitu usichostahili kupewa"uaminifu".

Kwa uaminifu chochote hufanikisha, imani yao kwako ndio mwanzo wa yote, fikra zao kwako ndio muendelezo wa yote, mafanikio yao kupitia wewe ndio mafanikio yako wewe. Uamuzi ni wako kufanikisha kwa kujenga ama kufanikisha kwa kubomoa. Safari hii sio lelemama, inahitaji upeo wa kuona mbali, kutazama zaidi ya ulipotoka na ulipo. Safari ya kujua nini kinachohitajika lakini kimekosekana, safari ya kuacha fikra mimi na kufuata fikra wao ndani ya mimi.

Wengi wao watafurahia na kukupongeza kwa hatua uliyofikia, na baadhi yao wataenda kinyume nao, ila wewe unajionaje?, unaweza ukaonekana paka mbele za watu lakini kumbe wewe ni simba! Au ukaonekana simba kumbe wewe paka! Wewe ama wao?, heshima bora huja baada ya dharau. Wewe unataka ipi?

Nilipogundua kua naweza kusema siwezi, nikajiuliza je ni siwezi kusema naweza au naweza kusema siwezi? Hapo ndipo nilipochanganyikiwa, nikaona nifanye kwanza kisha matokeo yatadhihirisha kua naweza ama siwezi?

Je naweza? Je siwezi? Haya ni maneno tu, vitendo ndio vina majibu sahihi, anayekuambia kua hauwezi ni yeye aliyesema sio wewe! Amua kwakua mimi najua unaweza kwakua mimi nimeweza basi hata wewe unaweza. Kumbuka wote tuko chini ya jua, wote tuko chini ya mwanga unaotuongoza. Tambua unachokipenda kukifanya, kisha fanya unachokipenda kwa moyo wako wote(100% ),weka firka zako zote, weka nguvu zako zote. Gusa kiini cha uwezo wako kwa nia moja ya kwamba unaweza, umeweza na utaweza. Mwanzo huwa ni mgumu kwakua hatujui mwisho utakuaje!..ndio maana kunakitu kinaitwa Tumaini..usipoteze Matumaini, usikate tamaa kamwe, ukianza anza hakuna kurudi nyuma,ukiteleza amka jipanguse kisha endelea..hatuviiti vikwazo bali ni changamoto na huu ndio utamu wa safari hii..mpaka hapa nilipofika katika safari hii ni changamoto ndio zimenijenga kutoka siwezi mpaka naweza....hata wewe ukiamua utaweza kwakua hakuna kinachoshindikana chini ya jua..Kumkichwa ni wewe!

DUNIA RANGI RANGILE ( 3 ) Sehemu ya Tatu

Sehemu ya Tatu
                                            
                            Mtunzi: Lasima Nassoro 
Wiki iliyopita tuliona kibe alivyifika mjini kwa Kanjubai, sasa yuko safarini anapelekwa eneo lake la kazi, je ni wapi na ni kazi gani,ungana na Mtunzi wako Lasima Nassoro kwa uhondo zaidi...
   Asubuhi na mapema walianza tena safari, walisafiri mchana kutwa. Walipita sehemu iliyokuwa kama jangwa, haikuwa na miti isipokuwa miba na miamba hadi wakafika katika msitu mkubwa. Ilipotimu saa tano usiku walifikia nyumba iliyokuwa katikati ya msitu mnene, Moris akamuambia Kibe,
"tumefika, nisubiri hapa, niende nikaangalie kama huyu jamaa yupo".
Geti lilikuwa limefungwa, akaamua kupanda ukuta ili aweze kuingia ndani, aliporuka ukuta akakutana na mbwa wakali, wale mbwa wakaanza kubweka huku wakitaka kumrarua. Lio akiwa chumbani kwake, akachukua bastola yake, akahakikisha kuwa ina risasi, akaenda dirishani kuchungulia nje, akaaona jamaa aking'ang'ana kupambana na mbwa, akaamua kutoka kupitia mlango wa nyuma, akanyata hadi alipomfikia yule jamaa, akamuwekea bastola ya kisogoni na kumuambia,
"leo utajua kilichomtoa Kanga manyoya". Moris aliposikia sauti ya Lio, akacheka,
"hahaha, Lio, Lio, Lio"
Lio baada ya kugundua kuwa mtu aliyevamia nyumba yake ni boss wake, naye akacheka kisha akamuambia,
"boss, una bahati niliamua kutoka, maana nilitaka niiachie risasi nikiwa ndani, bahati hukuwa katika tageti, imekuaje unafika saa hizi, halafu unaruka ukuta?"
Moris akavuta pumzi ndefu kisha akasema,
"nilijua umelala, naninavyokujua huwa ukilala kuamka ni shughuli pevu, ndio maana nikaamua
kuruka ukuta, hawa mbwa kidogo wanitoe roho".
"wanakufahamu hawa, walikuwa wanakutisha tu ili na mimi nitoke huko ndani, hujanijibu kuwa wafanya nini hapa saa hizi?".
"kuna dogo nimemleta, afanye kazi huku".
"kila idara mbona ina watu wa kutosha?".
"muweke kule kwenye vinu, baadae ukiona kuwa ni kijana muaminifu, unaweza ukamhamisha na kumpeleka kitengo kingine, huyo dogo nimemtoa kwa mkuu, yeye ndie aliyeniambia nimlete".
"sasa yuko wapi?"
"nimemuacha hapo nje ya geti, yupo garini"
Morisi akafungua geti na kwenda kuingiza gari, walipofika ndani, Morisi akamuambia Lio,
"Lio, huyu ndio dogo mwenyewe, anaitwa Kibe, Kibe huyu anaitwa Lio, atakuwa boss wako hapa, yeye ndiye msimamizi wa shughuli zote huku".
Baada ya Kibe kusalimiana na Lio, Lio akamuambia,
 "natumaini utakuwa mchapakazi mzuri,maana huwa sipendi watu wavivu, kama wewe ni mvivu, ujue kazi za huku hazikufai" Kibe akajibu,
"kazi ndio niliyoifata huku, kwahiyo ni jukumu langu kufanya kwa bidii hilo lililonileta hapa".
Lio akamgeukia Moris, "huko mlikotoka si mmekula?".
Moris akatabasam kisha akasema, "kwani wewe ni mgeni wa barabara ya kujia huku? huo mgahawa au hoteli itakuwa inaendeshwa na nyani au sokwe? maana hao ndio waliojaa njia yote".
"haya boss, nilifikiri mmepika huko njiani, ngoja niangalie chakufanya".
Lio akaenda jikoni kwake na kurudi akiwa amebeba sahani mbili zilizojaa wali na nyama, moja akampa Moris na nyingine Kibe, akawaambia,"hiki ndicho kilichopo, kwanza ni bahati tu niliamua kupika kingi, msiposhiba mutajazia na maji".
"tutashiba, na hii nyama ni aina gani?" hayo yalikuwa maneno ya Moris.
"we kula, usitake kujua ni aina gani ya nyama, ulifikiri tunafuga huku?".
"nafahamu kuwa hakuna mfugo hapa, nilitaka tu kujua ni aina gani ya nyama pori?".
"hiyo ni nyama ya swala".
"ooh! ndio maana tamu sana, bado umebakisha nyingine?".
"una maana gani, sinimekuambia hakuna chakula kingine zaidi ya hicho?"
"namaanisha kuwa kama una akiba ya nyama ya swala anigawie kesho nikiondoka nipeleke kwangu".
"hiyo utapata, lakini imekaushwa"
"safi sana, hiyo ndio nzuri, ukiipika hiyo uiunge vizuri na tui zito la nazi halafu upate na ugali mlaini na pilipili, hapo utatolewa mezani".
"hahaha, unapika mwenyewe? au kuna shemeji anayekupikia?"
"shemeji atoke wapi bwana, nilipokuwa mdogo mama yangu alinifunza kupika, kwahiyo nafurahia kupika nikitumia ujuzi nilioupata toka kwa mama yangu".
Wakati wote huo Lio alipokuwa anaongea na Moris, Kibe alikuwa kimya huku akimchunguza Lio alivyo, Lio alikuwa pandikizi la mtu, mweusi na alikuwa na mapengo, meno matatu au manne ya mbele hayakuwepo, halafu alikuwa ametoboa sikio la kushoto na alikuwa amevaa hereni, mkono wake
wa kushoto alikuwa amechora nge. Kibe akaanza kuingiwa na wasiwasi baada ya kumuangalia na kumchunguza Lio kwa muda, akawa na mawazo kuwa pengine hawa watu wanajihusisha na
biashara haramu maana kama ingekuwa halali, kwanini inafanyika katikati ya msitu mnene, ila hakutaka kuonyesha hofu yake maana japo hajakaa na Lio kwa muda mrefu, roho yake haikuwa na imani dhidi ya Lio, alimuona kuwa ni mtu ambaye anaweza kumtoa mtu roho. Baada ya kumaliza kula, Kibe akaonyeshwa sehemu ya kulala, huku akiambiwa kuwa kesho yake ndio atapelekwa katika kituo chake cha kazi. Baada ya kupanda kitandi, akafumba macho na kuomba mizimu ya kwao imulinde na chochote kibaya. Asubuhi na mapema, Lio alimuamsha Kibe, akamuonyesha maji ya kunawa uso, kisha akapewa uji.
"kaka Moris yuko wapi?" Kibe alimuuliza Lio.
"ameondoka kitambo sana , amesema anataka awahi kufika mjini maana kuna kazi nyingi sana zinamsubiria, maliza uji haraka twende maana saa zinakwenda. Alipomaliza kunywa uji, Lio akamuambia Kibe atoke waende, wakapanda gari aina ya Land Rover kisha wakaelekea juu mlimani, Kibe akamuuliza Lio,
"hicho kituo cha kazi kipo mbali sana?".
"ukienda kwa gari sio mbali sana, ila kwa mguu ni mbali kiasi".
"sasa nikishaanza kazi, nitakuwa nafikaje huko kwa  wakati? kama mtu akienda kwa mguu ni mbali".
"utakuwa unakaa huko huko pamoja na wenzako".
Walipofika juu mlimani, Kibe akaona nyumba zilizojengwa kwa miti na kuezekwa kwa nyasi, kisha akaona watu wasiopungua kumi, kila mmoja akiwa na kinu na mtwangio mkononi huku wakitwanga. Lio akasimamisha gari, akamuambia Kibe kuwa ashuke maana hapo ndipo  atakapofanyia kazi. Wale watu walipoona gari limesimama, wakaacha kutwanga na kulifuata lile gari, kijana mmoja aitwae Twalibe, akamsalimia Lio kasha Kibe, akamuuliza Lio,
"boss,leo mbona umetutembelea asubuhi subuhi kuna nini?". Lio akafungua mlango wa gari akashuka akasema,
 "nimewaongezea mtu mwingine maana nimeona kazi zinawalemea".
"tutashukuru sana boss, ndiye huyu?"
"yah, ndiye huyu anaitwa Kibe, Kibe hawa ni wafanyakazi wenzako, watakuonyesha namna ya kufanya kazi na mtakapo maliza kazi jioni, watakuonyesha sehemu ya kulala, Twalibe, si kuna vinu vya akiba?".
"ndio boss, vipo, ashindwe tu mwenyewe".
"haya mpeleke umuonyeshe vinu vilipo, kazi iendelee, nitarudi jioni kuangalia mlipofikia".
Lio akarudi katika gari kisha akaondoka. Twalibe akampeleka Kibe chumba ambacho vinu vimewekwa, wakachukua kinu kimoja na mtwangio wake, Kibe akamuuliza Twalibe,
"ni kitu gani kinatwangwa?".
Twalibe akamjibu,
"kuna majani fulani huwa yanaletwa hapa kila jioni, kazi yetu ni kuyatwanga kisha jioni boss analeta mengine na kuchukua yale yaliyotwangwa,t wende nikakuonyeshe yalipo ili uanze kazi".
Kibe akapelekwa chumba kingi kilichojaa magunia yaliyojaa majani, wakachukua gunia moja na kuelekea sehemu ile ambayo wenzao walikuwa wakiendelea kufanyia kazi.
Wakati wanaendelea kufanya kazi, Twalibe akamuuliza Kibe,
"kwani wewe umetokea wapi?".
Kibe akamjibu, "nimetokea kijiji kiitwacho SISI KWA SISI, ulishawahi kukisikia?".
"hapana, mie nimekulia mjini , sijawahi kufika kijijini".
"kwani ulikosa kazi nyingine huko mjini hadi uje kufanya kazi huku porini?".
"mie sijasoma,kama mtu umesoma na una vyeti vyako,hapo ndio utapata kazi za ofisini, ila watu kama sisi, kazi za mikono ndio saizi yetu, si umewahi kusikia kwa mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe?".
"sawa, sasa haya majani yana kazi gani?".
"mie sijui na sitaki kujua,ninachojua ni kuwa mwezi ukiisha Napata mshahara, kama haya majani wanauza au la, wanajua wenyewe".
Kibe akaamua kutouliza maswali zaidi, alijua kuwa wakati utafika ambapo majibu ya maswali yanayomtatiza atayapata. Walifanyakazi hadi muda wa chakula cha mchana ulipofika. Wakati wanaendelea kula, Kibe akamuuliza Twalibe,
"hiki chakula tunatakiwa tulipie?".
"la hasha, chakula na malazi ni juu ya muajiri, boss hapendi wafanyikazi wake wapate tabu".
"na mshahara ni mzuri au kiasi kidogo tu".
"kwa mtu ambaye hana kisomo na ukilinganisha na kazi tunayofanya, zinatutosha kusukuma maisha yetu, ila kwa yule ambaye hana mpangilio wa maisha anaweza kusema hazimtoshi".

Je haya ni majani gani? nini hatima ya Kibe? je nini kitamtokea kibe wakati yuko mbali na nyumbani kwao?...itaendelea wiki ijayo...