Friday, July 20, 2012

Vijana na Ujana-Mwisho/Vibaya na vibaya sana (Nimejaribu nimeshindwa kutoka)



             Kundi hili ni la wale vijana wanaopenda kujaribu vitu venye kuhatarisha, kundi lililo karibu na maji ya moto na lililo makini kwani linajitambua kua maji haya ni ya moto na yanaweza kuwaunguza wakati wowote, kundi hili liko bora ila sio sana na hapenda kuutumia Ujana wao kwa mambo kwa kujaribu ili kujua kipi chenye kufaa na kipi kisichofaa kwa manufaa ya baadae ya maisha yao, lakini kundi hili hujaribu kisha hushindwa kuacha walichojaribu ingawa kinahatarisha.

Kundi hili huendesha maisha yao vile nafsi zao zinataka.

Kundi hili halina fikra za mara mbili pale wanapotaka kufurahia maisha yao.

Kundi hili pia ni wazuri kwa kujitetea kwamba wanachofanya kina faida maishani mwao kwakua hisia na fikra zao huwa zimeshatekwa na kitu hicho.

Kundi hili pia huona fahari kufanya wanachikafanya kwakua wanakua wao na hawana haja ya kujificha kua hawafanyi. Ni moja kati ya kitu kizuri kwa kundi hili ni wakweli mbele ya nafsi zao.

Kundi hili hukubaliana na hali halisi ya kua nafsi zao zimeshindwa kushindana na matakwa ya nafsi.

 Changamoyo wanazokutana nazo:-
“Stay Away from him/her””kaa mbali nae”Moja ya changamoto ni kutengwa na wale wanaowapenda kutokana na msimamo wa kundi hili kushikilia wanachokifanya kua ndio bora kwao kwa wakati huo.

“Bird of the same feather””ndege wafananao”Kujichanganya kwao na watu ni kwa mashaka kwani huwa wanahisia kila mtu anawazungumzia wao. Huwa ni wagumu kuamini mtu labda wapate mtu aliye katika kundi lao ili waruke pamoja.

“Have change””nimebadilika”kundi hili hata kama likifanikiwa kubadilika hupata wakati mgumu sana kukubalika tena na wana jamii kwamba ni watu wa kawaida kama wengine. Hujikuta wanarudi tena walipotoka kutokana na kauli rejeo za jamii kwamba wanazuga au wanajidai wamebadilika. Ila kiukweli huwa wanabadilika.

Ushauri wangu kuhusu kundi hili
Hakuna kinachoshindikana chini ya jua, ingawa ni furaha na ni raha kufurahia maisha tofauti na wengine ila umakini katika kitu unachokifanya ni muhimu kwani kama hautajiumiza wewe mwenyewe basi ujue utawaumiza wale walio karibu na wewe.

Ndio ni halali yako kufanya unachopenda ila je tumeumbwa ili tuwe wabinafsi?. La hasha ni fikra zetu na nafsi ndizo zinatufaya tuwe hivyo..na pia ni rahisi kwa wao kutuelewa ila ni vigumu kwa wao kutufanya sisi tuwe wabora.

Kitu cha kuzingatia ni kutochanganya malengo yetu na hatari tunazotaka kuzijaribu. Hatari nyingine zinavutia kweli na zinatufanya tufurahie pale tunapozifanya ila kwa ndai nafsi inajaribu kupingana na hali hiyo kua “unajua unachokifanya sio sawa kwako ila hauna nafasi ya kuacha kukifanya kwa wakati kuo  kwakua nia kinaleta faraja, matumaini na furaha kwa wakati huo ila baada ya hapo ni maji ya moto”.


            Kwa ujumla maisha yana changamoto nyingi sana, na kwa vijana ni mara mbili ya changamoto hizo. Ukishafikisha umri wa kuanza kujitegemea kwa kijana kichwa huwa kiko katika hali ya mabadiliko transicion ambapo majukumu yanapokuwa juu yako na wewe unalazimika kukubaliana na majukumu hayo , na ndipo kijana hufikiria ni bora apate kitu cha kumpunguzia msongamano wa mawzo ili apate kutazama na kuchanganua nini kinakuja mbele yake. Hivyo kauli moja ya vijana ni “life Is short banaa lets us have fun”…je unajua ni majuku gani hayo? Je unajua umri wako na unachotakiwa ukifanye? Je unatambua kua umeshapiga hatua kadhaa kutoka pale ukipo na je unaelekea wapi na je umetazama hatua zako? Usikose sehemu ya pili ya makala hii ya “Vijana ja Ujana” ya "Tambua umri wako na majukumu muhimu kwako"…unataka uje uwe nani? na umejiaandaaje?usikose mfululizo huu wa a,e,i,o,u..amka,elimisha,imarisha,okoa na unganisha…kumbuka KUMKICHWA NI WEWE.

No comments:

Post a Comment