Tuesday, July 31, 2012

Ondoa Facebook Timeline kwa Profile yako

Facebook Timeline

              Timeline ni mtindo mpya wa muonekano wa kurasa ya mtumiaji wa facebook, ambayo huonesha vitu muhimu kama picha ama tukio jipya ambalo huonekana kwa mfumo wa hadithi ya mtu. Mtindo huu mpya ulianza kuonekana mwaka 2011..ambapo kwa wale waliokua mfumo wa zamani walitakiwa kuutazama(preview)mfumo huo mpya kisha kama utawavutia basi mtu huyo hukubaliana nao na kuanza matumizi yake..
 

Faida za Timeline..
Ni kwamba unaweza uka ongeza habari au ukaificha kabla mtu yoyote hajaiona.
Kugundua vitu na kuchangia(share) na wenzako
Kukusanya matukio yako muhimu kwa pamoja
Kusikiliza mziki kwa facebook
n.k
                             

             Tatizo lililo jitokeza ni kwamba mtindo huu umewachosha watu wengi sana, na wengi wao wanataka kuondokana nao..lakini kwa namna ilivyowekwa ni kwamba hauwezi kuondokana na mtindo huo..ila unaweza ukaondokana nao kwenye Browser yako peke yako..ila kwa wale watakaotembelea ukuta(WALL) yako watakuta Timeline kama zamani.

            Hivyo ningependa kuwashauri ambao tayari wameshaingia kwenye mtindo huu basi wauvumilie tu…kwakua kuna baadhi ya mitandao inayotoa taarifa kua unaweza kuondokana na Timeline, kisha wanakupa link ya kuifata..link hizo zinaweza kua virusi(virus)..hivyo ningewashauri na wale ambao bado hawajaingia kwa Timeline..wasiingie huku kama watataka kutoka…huu ndio ujanja wa mitandao ya kijamii…ukishaingia ni ngumu kutoka.
 

             Tafadhali Changia makala hii na marafiki zako wanaousumbiliwa na Timeline, Pia usisahau kutoa maoni yako na ushauri, kama una maswali hii ndio sehemu ya kuuliza…kumbuka Kumkichwa ni wewe!

No comments:

Post a Comment